Droo ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika 2025/2026 | CAF Confederation Cup Groups 2025/2026
Droo ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika CAF 2025/2026 imefanyika rasmi jijini Johannesburg, Afrika Kusini, ikishuhudia vilabu vikubwa barani humo vikigawanywa katika makundi manne yenye ushindani mkubwa.
Hafla hiyo iliongozwa na nyota wa zamani wa soka la Afrika, Alexandre
Song kutoka Cameroon na Christopher Katongo kutoka Zambia, ambao
walisisitiza umuhimu wa mashindano haya katika kukuza ubora wa soka la
vilabu barani Afrika. Katika droo hiyo, vilabu vinne kutoka Morocco
vilipata nafasi ya kushiriki hatua ya makundi RS Berkane na AS FAR
wakicheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, huku Wydad AC na Olympic
Club Safi wakipewa nafasi ya kutetea heshima ya taifa hilo katika Kombe
la Shirikisho Afrika CAF 2025/2026.
- Ratiba ya Mechi Zote Makundi Klabu Bingwa CAF 2025/2026 | CAF Champions League 2025/2026 Fixtures
- Ratiba ya Mechi Zote za Makundi Kombe la Shirikisho Afrika 2025/2026 | CAF Confederation Cup 2025/2026 Fixtures
- Miguel Gamondi Ateuliwa Kuinoa Taifa Stars kuelekea AFCON 2025
- Bodi ya Ligi ya TPLB: Taarifa Muhimu Kuhusu Ligi Kuu ya NBC
- Makundi ya Klabu Bingwa Africa 2025/2026 | Caf Champions League Groups 2025/2026
- Msimamo wa NBC Premier League Tanzania
- Msimamo Championship Tanzania
- Ligi 10 Bora Duniani | FIFA Ranking
- Top 10 ya Viungo (Midfielders) Bora Duniani
- Ijue Simba Historia ya Simba SC
- Soweto Derby History – Top Derby in Africa
Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF 2025/2026
Kundi A
- USM Alger (Algeria)
- Djoliba AC (Mali)
- Olympic Club Safi (Morocco)
- FC San Pedro (Ivory Coast)
Kundi B
- Wydad AC (Morocco)
- AS Maniema (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo)
- Azam FC (Tanzania)
- Nairobi United FC (Kenya)
Kundi C
- CR Belouizdad (Algeria)
- Stellenbosch FC (Afrika Kusini)
- AS Otoho (Congo)
- Singida Black Stars (Tanzania)
Kundi D
- Zamalek SC (Misri)
- Al Masry SC (Misri)
- Kaizer Chiefs (Afrika Kusini)
- Zesco United FC (Zambia)
Fursa kwa Vilabu vya Afrika Mashariki
Kwa mara nyingine tena, timu za Afrika Mashariki zimepata nafasi ya kuonyesha uwezo wao. Azam FC na Singida Black Stars kutoka Tanzania, pamoja na Nairobi United FC ya Kenya, zote zipo kwenye hatua ya makundi ishara kwamba maendeleo ya soka katika ukanda huu yanaendelea kwa kasi. Wadadisi wa soka barani wamesema kuwa mwaka huu unaweza kuwa “mwaka wa Afrika Mashariki,” kutokana na idadi ya timu kutoka eneo hilo kufikia hatua ya makundi katika michuano yote ya CAF.
Ratiba na Matangazo
Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka CAF, mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF 2025/2026 yataanza
rasmi tarehe 21 Novemba 2025. Mashabiki wataweza kufuatilia mechi zote
moja kwa moja kupitia vituo vya televisheni Arryadia na beIN Sports, ambavyo vimepata haki za matangazo ya michuano hii.
.png)


No comments:
Post a Comment